Watu 17 wauawa katika mashambulizi ya anga mpakani mwa Sudani na Sudani Kusini

Watu kumi na saba wamepoteza maisha kusini mwa nchi ya Sudan mpakani mwa nchi hiyo na Sudan Kusini kufuatia shambulio la anga lililofanywa na majeshi ya Sudan.
Msemaji wa wa majeshi ya Sudan Kusini Philip Aguer, amesema kuwa serikali ya Khartoum imeendelea kupeleka vikosi vyake mpakani mwa nchi hizo mbili kwenye maeneo yenye mgogoro na kwamba imekuwa ikifanya mashambulizi dhidi ya raia.
Kufuatia tuhuma hizo za Sudan Kusini, serikali ya khartoom kupitia msemaji wa jeshi la nchi hiyo Al Sawarmi Khalid amekanusha majeshi ya nchi hiyo kufanya mashambulizi yoyote siku ya alhamisi yaliyolenga raia wa kusini badala yake amesema kuwa jeshi lake limebaini kuwa wapiganaji zaidi ya 350 wanaopigana vita katika jimbo la darfur wameingia sudan kusini kupitia mpaka huo.
Mashambulizi hayo yameendelea kuzusha hali ya sintofahamu kuhusu uhusiano kati ya nchi hizi mbili ambazo zimekuwa zikigombea eneo la mpaka wa abyei ambako hivi sasa vikosi vya umoja wa mataifa vya kulinda amani vimepelekwa.







MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya