Makala iliyochapishwa tarehe : Jumanne 22 mei 2012 -
Taarifa za ivi karibuni : Jumanne 22 mei 2012
Mwanamke wa kwanza aula FIFA ni raia wa Burundi
Rais wa FIFA Sepp Blatter
REUTERS/Arnd WiegmannShirikisho la soka duniani, FIFA limemteua Lydia Nsekera kuwa mwanamke wa kwanza kwa kamati yake kuu ili kuimarisha safu ya uongozi katika shirikisho hilo.
Mpaka anateuliwa kushika nafasi hiyo, Lydia Nsekera ni rais wa shirikisho la soka la Burundi.
Mwanamama huyo ambaye amepewa heshima kubwa kimichezo atashikilia wadhifa huo mpya kwa mwaka mmoja hadi utakapofanyika uchaguzi rasmi mwaka 2013.
Katika hatua nyingine shirikisho hilo limemteua raia mmoja kutoka Uswisi Domenico Scala kuongoza kamati mpya ya uhasibu inayolenga kusimamia matumizi ya FIFA.







MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya