Makala iliyochapishwa tarehe : Jumanne 22 mei 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Jumanne 22 mei 2012

Mwanamke wa kwanza aula FIFA ni raia wa Burundi

Rais wa FIFA Sepp Blatter
REUTERS/Arnd Wiegmann

Na Victor Robert Wile

Shirikisho la soka duniani, FIFA limemteua Lydia Nsekera kuwa mwanamke wa kwanza kwa kamati yake kuu ili kuimarisha safu ya uongozi katika shirikisho hilo.

Mpaka anateuliwa kushika nafasi hiyo, Lydia Nsekera ni rais wa shirikisho la soka la Burundi.

Mwanamama huyo ambaye amepewa heshima kubwa kimichezo atashikilia wadhifa huo mpya kwa mwaka mmoja hadi utakapofanyika uchaguzi rasmi mwaka 2013.

Katika hatua nyingine shirikisho hilo limemteua raia mmoja kutoka Uswisi Domenico Scala kuongoza kamati mpya ya uhasibu inayolenga kusimamia matumizi ya FIFA.

tags: Burundi - Sepp Blatter
MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close