Guinea Bissau-Cote D' Ivoire - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumatano 23 mei 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Jumatano 23 mei 2012

Vikosi vya Guinea Bissau kurejea kambini, Rais Ouatara amfukuza kazi waziri kwa rushwa

Rui Duarte Barros Waziri mkuu wa Guinée Bissau
ALFA BA / AFP

Na Victor Robert Wile

Vikosi vya Guinea Bissau vimeapa hii leo kurejea katika kambi zao baada ya Mamlaka ya mpito kuunda Serikali mpya iliyohusisha afisa wa kijeshi aliyeshiriki mapinduzi ya Aprili 12 nchini humo.

Rais wa Mpito wa Guinea Bissau, Serifo Nhanadjo alitia saini makubaliano ya kuunda baraza lenye mawaziri 27 chini ya waziri mkuu Rui Duarte Barros, akiwemo waziri wa ulinzi Kanali Celestino Carvalho, mmoja wanajeshi waliomuondoa Rais wa nchi hiyo madarkani.

Msemaji wa majeshi yaliiongoza mapinduzi, kanali Daba Na Walna ameliambia shirika la habari la ufaransa kuwa hivi sasa watarejea kambini kwa kuwa Serikali ya mpito imepatikana.

Siku ya jumamosi majeshi, Bunge na vyama vya kisiasa vilitia saini makubaliano ya kutafuta namna ya kumaliza vurumai zilizosababishwa na mapinduzi.

Miongoni mwa makubaliano hayo ni pamoja na uundwaji wa tume ya uchaguzi,ambapo itaongozwa na jaji ambaye atazipitia tena sheria za uchaguzi.

Wakati huohuo Rais wa Cote D ivoire, Allasane Ouatara amemfuta kazi waziri wa masuala ya Uhusiano wa Afika Adama Bictogo akishutumiwa kujihusisha na vitndo vya Rushwa.

Ofisi ya Rais imesema Ouattara amemfuta kazi rasmi Bictogo aliyekuwa akihudumu kwenye serikali yake.

Kwa mujibu wa gazeti la Jeune Afrique la nchini Cote d ivoire, Bictogo kwa kufanya dhuluma ya malipo ya watu walioathirika na sumu iliyomwagwa Baharini na Meli ya mizigo jijini Abidjan

Bictogo pia, alikuwa miongoni mwa wajumbe wa ECOWAS walio na kibarua cha kutatua mzozo wa kisiasa nchini Mali.

 

 

 

 

 

tags: Alassane Ouattara - Côte d’Ivoire - Guinea-Bissau
MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close