Pata taarifa kuu
ICTR-RWANDA-Sheria

ICTR yathibitisha hukumu ya kifungo cha miaka jdela kwa Agustin Bizimungu

Mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita inayoshughulikia kesi za mauaji ya kimbari iliyoko mjini Arusha ICTR, hapo jana imethibitisha hukumu ya kifungo cha miaka 30 jela kwa aliyekuwa mkuu wa majeshi wa Rwanda wakati huo, Augustin Bizimungu.

Sehemu ya ukumbusho wa mauwaji ya kimbari yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994.
Sehemu ya ukumbusho wa mauwaji ya kimbari yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994. REUTERS/Noor Khamis
Matangazo ya kibiashara

Jaji aliyekuwa anasikiliza rufaa iliyokatwa na Bizimungu, Jaji Theodor Meron amesema upande wa utetezi haukuwasilisha ushahidi wa kutosha kuunga mkono rufaa yao na kwamba mahakama imemkuta na hatia ya makosa ya kuchochea mauaji ya kimbari dhidi ya jamii ya watu wa Kitutsi.

Mahakama hiyo pia imemkuta Bizimungu na hatia ya kosa la kutoa hotuba iliyoelekeza kutekelezwa kwa mauaji ya Watutsi siku chache kabla ya yeye kutangazwa kama mkuu wa majehsi ya Rwanda mwaka 1994.

Wanamgambo wa kihutu wakiwa katika mazoezi , Julai 27 mwaka 1994 mjini Butare, nchini Rwanda.
Wanamgambo wa kihutu wakiwa katika mazoezi , Julai 27 mwaka 1994 mjini Butare, nchini Rwanda. AFP / HOCINE ZAOURAR

Wachambuzi wa mambo wanaizungumziaje hukumu aliyopewa Bizimungu anayedaiwa kuwa kinara wa mauaji ya kimbari mwaka 1994? Tom Ndahiro anazungumza nasi akiwa mjini Kigali Rwanda.

mkutano wa pili wa kimataifa juu ya utawala na demokrasia barani Afrika, Asia na Mashariki ya kati waanza mjini Kigali nchini Rwanda.
mkutano wa pili wa kimataifa juu ya utawala na demokrasia barani Afrika, Asia na Mashariki ya kati waanza mjini Kigali nchini Rwanda. Arthur Buliva/CC/wikimedia.org

Hayo yakijiri mkutano wa pili wa kimataifa juu ya utawala na demokrasia barani Afrika, Asia na Mashariki ya kati ulianza jana mjini Kigali nchini Rwanda.

Mkutano huo umekuja huku demokrasia na utawala bora katika nchi zinazoendelea vikikumbwa na changamoto kedekede.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.