Pata taarifa kuu
LIBYA-Usalama

Libya : wapiganaji waendelea kudhibiti kambi za kijeshi

Kambi kuu ya kikosi maalum jijini Benghazi nchini Libya imedhibitiwa na kundi la wapiganaji wa kiislamu baada ya siku kadhaa za makabiliano mashariki mwa Libya, maafisa wamethibitisha.

Kikosi maalum cha Benghazi chatimuliwa na makundi ya wapiganaji.
Kikosi maalum cha Benghazi chatimuliwa na makundi ya wapiganaji. REUTERS/Esam Omran Al-Fetori
Matangazo ya kibiashara

Kutokana na hali hiyo, Ufaransa inapanga kwa namna yoyote kuwaondoa raia wake nchini Libya kupitia njia ya majini, baada ya uamzi uliyochukuliwa na mataifa ya magharibi ikiwemo Marekani, Uholanzi, Canada na Bulgaria, ya kuwaondoa maafisa wa balozi zao nchini Libya.

Mataifa mengi yamewataka raia wao kuondoka chini Libya, ambako kunashuhudiwa mapigano tangu wiki mbili zilizopita kati ya makundi ya wapiganaji katika mji ya Tripoli na Benghazi.

Mapigano yanaendelea katika mji wa Benghazi,Julai 27 mwaka 2014.
Mapigano yanaendelea katika mji wa Benghazi,Julai 27 mwaka 2014. REUTERS/Esam Omran Al-Fetori

Chanzo cha kijeshi , kimefahamisha kwamba kwamba kambi hiyo kuu ya kikosi maalum imedhibitiwa tangu jumanne wiki hii jioni na makundi ya wapiganaji wa kislamu likiwemo kundi la Ansar Asharia, ambalo liliwekwa na Washington kwenye orodha ya makundi ya kigaidi.

Kundi la Ansar Asharia limeweka picha za wapiganaji wake na silaha walizokamata kwenye ukurasa wake wa facebook.

Libya inakabiliwa na hali ya kukosekana kwa utulivu tangu mapiganao ya 2011 yaliyomtimua madarakani rais Moamar Al Kadhafi, huku baadhi ya maeneo ya nchi yakidhibitiwa na wanamgambo.

Afisa wa Vikosi Maalum vya libya, Fadel al-Hassi Amewaambia waandishi wa habari jana jumanne kuwa wamejiondoa katika kambi ya kijeshi ya Benghazi baada ya mashambulizi makali ya makombora.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.