Pata taarifa kuu
NIGERIA-BOKO HARAM-Usalama

Nigeria: polisi yaanzisha zoezi la kuwatafuta askari polisi 20 waliotoweka

Askari polisi ishirini wametoweka kwa kipindi cha majuma matatu sasa baada ya kundi la wapiganaji wa Boko Haram kushambulia kituo cha mafunzo nje kidogo ya jiji eneo la kaskazini mwa Mji wa Gwoza. afisa mkuu wa Polisi amethibitisha.

Maafisa wa jeshi la ulinzi nchini Nigeria wakikagua eneo la Kirenowa ambalo limekua likitumiwa na Boko Haram kama makao makuu yake.
Maafisa wa jeshi la ulinzi nchini Nigeria wakikagua eneo la Kirenowa ambalo limekua likitumiwa na Boko Haram kama makao makuu yake. AFP Photo
Matangazo ya kibiashara

Hata hivyo Inspekta mkuu wa Polisi nchini Nigeria, général Suleiman Abba amewaambia wandishi wa habari kuwa polisi imeendelea na uchunguzi kubaini maeneo gani waliko.

Wakati hayo yanaarifiwa namna hiyo mtoto wa aliyekuwa Rais wa Nigeria, Olesugun Obasanjo amejeruhiwa kwa risasi wakati wa makabiliano makali na wapiganaji hao wa kiislamu Boko Haram.

Luteni Kanali Adeboye Obasanjo alijeruhiwa siku ya jumatatu wakati jeshi la Nigeria lilipokuwa likipambana kuudhibiti mji wa Michika karibu na mji wa Mubi mji uliokuwa ukidhibitiwa na wanamgambo katika jimbo la Adamawa.

Mashahidi wamesema kuwa maelfu ya watu wameyakimbia makazi yao, huku wanajeshi wakiondoka kwenye kambi zao. Inaarifiwa kuwa chuo kikuu katika jimbo hilo kimefungwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.