Mkutano wa AU: faili kubwa ziliyoandaliwa na Baraza la Mawaziri
Katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa, mkutano wa 24 wa marais na viongozi wa serikali wa Umoja wa Afrika (AU) utazinduliwa Ijumaa Januari 30.
Imechapishwa:
Kabla ya mkutano huo, rais wa bodi ya shirikisho hilo, Nkosazaba Dlamini Zuma, alikuwa ametoa wito kwa marais na viongozi wa serikali kulichukulia mikononi suala la Boko Haram.
Lakini masuala mengine kama vile hali ya usalam inayojiri Libya na Mali yamewekwa juu ya meza.
Mawaziri wa mambo ya nje wa nchi wanachama wa AU ambao wanakukutana tangu mwanzoni mwa wiki hii. Walikuwa na siku tatu ya maandalizi ya mkutano wa marais na viongozi wa serikali.
Kwa muda wa siku tatu, waliangazia kwa pamoja masuala mengi. Ajenda ya Baraza la mawaziri katika muhimili wake, lakini mikutano yote sambamba ambayo ilihamasisha wajumbe wengi.
Maandalizi ya faili kubwa
Kulikuwa na ripoti ya Mwenyekiti wa Kamati na Makamishna, ambayo inafanyika katika kila kikao cha Umoja wa frika, lakini pia ajenda 2063, ikiwa ni pamoja na faili muhimu kuhusu malengo ya Umoja wa Afrika kabla ya kuadhimisha miaka 100 tangu Umoja wa Afrika uanzishwe (AUO).
Kuna mpango unaolenga kuimarisha muungano wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika. Hii inaendana na utekelezaji wa miundombinu kadhaa katika nafasi ya wanawake katika siasa. "Uwezeshaji wa wanawake na maendeleo", na hio ndio kaulimbiu ya mkutano huu.
Katika ajenda ya mkutano huu, kuna kupitishwa kwa hitimisho la ripoti Obasanjo, ambayo imetimiza sasa miaka mitatu, inayoeleza uwezekano mpya wa fedha mbadala kwa ajili ya Umoja wa Afrika. Kwa sasa, asilimia 40 ya bajeti ya Umoja wa Afrika inatokana na michango ya nchi wanachama. Shirikisho hili linalojumuisha nchi za Afrika Pan linakabiliwa na ukosefu wa fedha za kutosha.
Mada nyingine kubwa, ni ile ya chaguzi katika taasisi mbalimbali za Umoja wa Afrika ambayo itakuwa mwenyeji wa mkutano wa kilele unaopangwa kufanyika hivi karibuni baada ya Chad kujiondoa.