Pata taarifa kuu
NIGERIA

Kura zinaendelea kupigwa nchini Nigeria leo Jumapili

Zoezi la upigaji kura linaendelea leo Jumapili katika vituo 300 kati ya Laki Moja na nusu nchini Nigeria.

Wapiga kura nchini Nigeria
Wapiga kura nchini Nigeria REUTERS/Goran Tomasevic
Matangazo ya kibiashara

Tume ya uchaguzi iliahirisha uchaguzi katika maeneo hayo kwa sababu ya hitilafu ya mitambo ya kutambua vitambulisho vya kupigia kura.

Msemaji wa Tume ya Uchaguzi Kayode Idowe amesema kuna maeneo mashine za kusoma kadi za kupigia kura hazikutumiwa kabisa kwa sababu ya hitilafu ya teknolojia.

Maafaisa wa Tume ya Uchaguzi INEC
Maafaisa wa Tume ya Uchaguzi INEC REUTERS

Rais Goodluck Jonathan pia aliathiriwa na tatizo hili na kulazimika kutimia njia ya kawaida kabla ya kupiga kura hapo jana.

Hata hivyo, katika maeneo ambayo zoezi hili lilikwenda vizuri kura zimeanza kuhesabiwa leo Jumapili.

Chama tawala PDP kimeishtumu Tume ya Uchaguzi kwa kutofanya maandalizi ya mapema kuhusu mitambo hii, huku muungano wa upinzani APC ukisisitiza umuhimu wa utumizi wa mitambo hiyo ili kuepuka wizi wa kura.

Mpigaji kura akitekeleza haki yake mjini Lagos
Mpigaji kura akitekeleza haki yake mjini Lagos REUTERS/Kunle Ajayi

Ushindani mkubwa ni kati ya rais Goodluck Jonathan na kigogo wa upinzani Muhamdu Buhari.

Wachambuzi wa siasa nchini Nigeria wanasema huu ndio uchaguzi wenye ushindani mkubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa katika taifa hilo tangu ilipojipatia uhuru wake mwaka 1960.

Uchaguzi huu uliahirishwa kwa muda wa wiki sita ili kutoa muda kwa jeshi la serikali na yale ya nchi jirani ya  Chad, Niger na Cameroon kupambana na kundi la Boko Haram Kaskazini mwa nchi hiyo.

Rais Jonathan na mpinzani wake Buhari wameahidi kuhakikisha kuwa ghasia hazitokei nchini humo wakati wa zoezi hili na baada ya upigaji kura na watakubali matokeo.

AFP/Pius Utomi Ekpei

Nigeria imefunga mipaka yake yote kwa sababu za kiusalama.

Marekani na mataifa mengine ya Magharibi yamewaomba wananchi wa Nigeria kutojihusisha na gahsia kama ilivyokuwa mwaka 2011 ambapo watu 800 walipoteza maisha.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.