Pata taarifa kuu
BURUNDI-AMNESTY INTERNATIONAL-MATESO-HAKI

Amnesty International yavituhumu vikosi vya usalama vya Burundi

Shirika la Kimataifa la kutetea haki za Binadamu la Amnesty International limesema maafisa wa usalama nchini Burundi wamekuwa wakitumia vyuma na tindikali dhidi ya wafuasi wa upinzani.

Mkazi wa Cibitoke akikimbia ghasia zilyozuka wakati wa operesheni ya polisi ya tarehe 1 Julai.
Mkazi wa Cibitoke akikimbia ghasia zilyozuka wakati wa operesheni ya polisi ya tarehe 1 Julai. AFP PHOTO / MARCO LONGARI
Matangazo ya kibiashara

Amnesty inasema ushahidi umeonesha kuwa polisi na maafisa wa ujasusi wamekuwa wakitumia mbinu hizo kuwalazimisha wafuasi wa upinzani kukiri taarifa wanazozitaka.

Polisi pia wameshtumiwa kuwapiga wafuasi hayo na nyaya za umeme na kuwalazimisha kuinamisha vichwa vyao ndnai ya maji chafu.

Mwanamume mmoja amesema alifungiwa dumu la mchanga katika sehemu zake za siri kwa nusu saa hadi akazirai.

Hata hivyo mauaji yamekithiri nchini Burundi hasa katika mji mkuu wa Bujumbura, ambapo watu wanauawa kila kukicha. hali hii imepelekea raia kuanza kukimbilia katika nchi jirani, husuan nchini Rwanda.

Je kuna raia wa Rwanda ambao hukamatwa Burundi?

Hivi karibuni serikali ya Rwanda imewaonya viongozi wa Burundi na kuwataka kuwaachilia huru raia wake wanaokamatwa na kupelekwa sehemu isiojulikana. Mashahidi wanasema kuna raia wa Rwanda ambao hivi karibuni walitereshwa ndani ya basi ziliyokua zikitokea Rwanda zikielekea Bujumbura. Mashahidi wengine wamebaini kwamba kuna vizuizi ambavyo vimewekwa katika eneo la Bugarama, mkoani Muramvya, ambapo kila gari ya uchukuzi inapofika sehemu hiyo abiria wote hullazimishwa kushuka na kuonyesha kadi zao za uraia, huku wakifanyiwa msako. Inaarifiwa kuwa vizuizi hivyo hulindwa na askari polisi na vijana ambao wanasadikiwa kuwa ni kutoka chama tawala cha CNDD-FDD, Imbonerakure.

Viongozi wa Burundi hawajaeleza lolote kuhusu onyo hilo kutoka Rwanda. hali ya wasi wasi imeendelea kutanda katika maeneo mbalimbali nchini Burundi.

Hayo yakijiri, idadi ndogo ya wapiga kura wamejitokeza Jumatatu wiki hii kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa, nchini Burundi.

Uchaguzi huu unakuja siku chache tu baada ya rais Piere Nkurunziza kuapishwa baada ya kushinda uchaguzi weenye utata uliokosolewa kimataifa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.