Pata taarifa kuu
AFRIKA KUSINI-OSCAR PISTORIUS-TUHUMA-HAKI

Wazazi wa Reeva Steenkamp wamshushia lawama Oscar Pistorius

Wazazi wa Reeva Steenkamp wanasema mwanariadha mlemavu Oscar Pistorius alimpiga risasi na kumuua binti yao kwa makusudi.

Oscar Pistorius aisabahi familia yake kabla ya kupelekwa jela, Oktoba 21 mwaka 2014.
Oscar Pistorius aisabahi familia yake kabla ya kupelekwa jela, Oktoba 21 mwaka 2014. REUTERS/Herman Verwey/Pool
Matangazo ya kibiashara

Wazazi wa Steenkamp wameimbia Runinga ya Australia maisha yao yamekuwa magumu na hawako tayari kuzungumza na Pistorius.

Wakitoa kauli hiyo kwa mara ya kwanza tangu kutolewa kwa hukumu ya Pistorius mwaka jana aliyehukumiwa jela kwa miezi kumi kwa kosa la kuua bila kukusudia na alitarajiwa kuachiliwa huru wiki iliyopita lakini Waziri wa haki Michael Masutha akabadilisha hatua hiyo.

Wazazi hao wamesisitiza kuwa uamuzi uliofanywa na Mahakama haukuwa sahihi.

Viongozi wa Mashtaka wiki iliyopita waliwalisha rufaa ya kutaka uamuzi wa Mahakama mwaka uliopita ubadilishwe na kumhukumu Pistorius kwa kosa la kuua kwa kukusudia.
Ikiwa uamuzi wa Mahakama iliyompa hukumu hiyo utabadilishwa huenda akafungwa jela miaka 15.

Siku ya mwisho ya kusikilizwa kesi ya Oscar Pistorius, ambapo Mwendesha mashataka aliomba kifungo cha miaka 10 dhidi ya mwanariadha huyo mlemavu, Oktoba 17 mwaka 2014.
Siku ya mwisho ya kusikilizwa kesi ya Oscar Pistorius, ambapo Mwendesha mashataka aliomba kifungo cha miaka 10 dhidi ya mwanariadha huyo mlemavu, Oktoba 17 mwaka 2014. REUTERS/Werner Beukes/Pool

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.