Pata taarifa kuu
BURUNDI-SIASA-USALAMA

Serikali mpya ya Burundi yaundwa

Hatimaye rais wa Burundi Pierre Nkurunziza ameunda serikali mpya yenye mawaziri ishirini, licha ya kuendelea kutengwa kimataifa.

Wakati wa kuapishwa kwake, Agosti 20, 2015, Pierre Nkurunziza ametangaza nia yake ya kuunda serikali ya umoja wa kitaifa.
Wakati wa kuapishwa kwake, Agosti 20, 2015, Pierre Nkurunziza ametangaza nia yake ya kuunda serikali ya umoja wa kitaifa. REUTERS/Evrard Ngendakumana
Matangazo ya kibiashara

Baraza hili jipya la mawaziri linaundwa na washirika wa karibu wa rais huyo, wengi wao ni wale waliohudumu katika mihula miwili iliopita.

Wizara muhimu zimepewa washirika wake wa karibu.

Alain Aimé Nyamitwe, kaka wa mshauri mkuu wa rais Nkurunziza,  anayehusika na mawasiliano, ameteuliwa kuwa waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa.

Pascal Barandagiye, aliyekuwa waziri wa sheria tangu mwaka 2010 hadi mwaka huu ameteuliwa kuwa waziri wa mambo ya ndani.

Alain Guillaume Bunyoni, aliyekuwa kipndi fulani waziri wa usalama na baadaye afisa anayehusika na safari za rais, ameteuliwa kuwa waziri wa usalama.

Waziri wa zamani wa ulinzi Emmanuel Ntahomvukiye, aliyeteuliwa hivi karibuni baada ya jenerali Pontien Gaciyubwenge kuachishwa kazi kwenye wadhifa huo, ameendelea kushikilia wadhifa wake.

Waziri wa zamani wa mambo ya jumuiya ya Afrika Mashariki, Léontine Nzeyimana, ameendelea kushikilia wadhifa wake.

Waziri wa zamani wa sheria baada ya uchaguzi wa mwaka 2010, Aimée Laurentine Kanyana, amerejeshwa kwenye wadhifa wake.

Waziri wa zamani wa fedha, Tabu Abdallah Manirakiza, ameendelea kushikilia wadhifa wake.

Janvière Ndirahisha, ameteuliwa kuwa waziri wa elimu ya msingi, sekondari, elimu ya juu na utafiti wa sayansi.

Déo Guide Rurema, ameteuliwa kuwa waziri wa kilimo na mifugo.

Nestor Bankumukunzi, ameteuliwa kuwa waziri wa posta, mawasiliano na teknolojia ya habari.

Emmanuel Niyonkuru, ameteuliwa kuwa waziri wa maji, mazingira na ujenzi wa miji.

Pélate Niyonkuru, ameteuliwa kuwa waziri wa biashara.

Josiane Nijimbere, ameteuliwa kuwa waziri wa afya.

Côme Manirakiza, ameteuliwa kuwa waziri wa nishati na madini

Serges Ndayiragije, waziri wa utawala bora.

Félix Mpozerirenga, waziri wa wafanyakazi, kazi na ajira

Jean Bosco Ntunzwenimana, waziri wa uchukuzi

Jeanne d’Arc Kagayo, waziri wa maendeleo ya wilaya

Waziri wa zamani wa utawala bora, Martin Nivyabandi, ameteuliwa kuwa waziri wa haki za binadamu, jamii, na jinsia

Jean Bosco Hitimana, ameteuliwa kuwa waziri wa vijana, michezo na utamaduni

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.