Pata taarifa kuu
UGANDA-SIASA

Mgombea kwa tiketi ya chama cha FDC kujulikana leo

Zaidi ya wajumbe elfu 1 wa chama cha upinzani nchini Uganda FDC wanapiga kura leo Jumatano kumchagua atakayepeperusha bendera ya chama hicho wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.

Raia wakijihusisha na shughuli zao mbalimbali katika mji wa Kampala, ambako kunafanyika mkutano mkk wa chama cha upinzani cha FDC kumchagua atakayepeperusha bendera ya chama hicho wakati wa uchaguzi Mkuu wa mwaka ujao.
Raia wakijihusisha na shughuli zao mbalimbali katika mji wa Kampala, ambako kunafanyika mkutano mkk wa chama cha upinzani cha FDC kumchagua atakayepeperusha bendera ya chama hicho wakati wa uchaguzi Mkuu wa mwaka ujao. RFI/Gloria Nakiyimba
Matangazo ya kibiashara

Kinyanyanyiro ni kati ya kiongozi wa zamani wa chama hicho Dokta Kizza Besigye na Mwenyekiti wa sasa Meja Jenerali Mugisha Muntu.

Besigye na Muntu wamekuwa wakichuana mara kwa mara kupeperusha bendera ya chama hicho na kwa nyakati zote Besigye ameibuka mshindi.

Wajumbe wa chama hicho wanasema wako tayari kumchagua mgombea wao baada ya miezi miwii ya kampeni kumalizika.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.