Pata taarifa kuu
MAREKANI-Usalama

Marekani : mji wa Ferguson waendelea kukumbwa na machafuko

Hali ya sintofahamu inaendelea kutanda katika mji wa Ferguson (Missouri) kufuatia maandamano yenye misingi ya rangi, amabyo yamesababisha watu wawili kujeruhiwa usiku wa jumatatu kuamkia jumanne wiki hii, huku watu 31 wakiwa wamekamatwa.

Kikosi cha ulinzi wa taifa kimetumwa katika mji wa  Ferguson, Agosti 18 mwaka 2014.
Kikosi cha ulinzi wa taifa kimetumwa katika mji wa Ferguson, Agosti 18 mwaka 2014. AFP PHOTO / Michael B. THOMAS
Matangazo ya kibiashara

Hivi karibuni rais wa Marekani Barack Obama, alitoa wito wa kukomesha maandamano hayo, akiitaka polisi kutotumia nguvu kwa kuwatawanya waandamanaji.

Wakaazi wFerguson, ambako Michael Brown, alikua akiishi.
Wakaazi wFerguson, ambako Michael Brown, alikua akiishi. REUTERS/Lucas Jackson

Mji huo mdogo ulioko katikati ya Marekani unakabiliwa na machafuko tangu askari polisi alipomuua kijana mweusi, Michael Brown, Agosti 9 katika mazingira ya kutatanisha.

Polisi imesema watu wawili wamejeruhiwa kwa risase ziliyofyatuliwa na waandamanaji.

“Wahanga wamejeruhiwa kwa risase ziliyopigwa kutokea upande wa waandamanaji”, mkuu wa polisi, Ron Johnson, ameambia vyombo vya habari, huku akibaini kwamba rais Obama ameitaka polisi kutotumia nguvu, na ndiyo maana polisi haijafyatua risase, na imetumia mabomu ya kutoa machozi katika dakika ya mwisho, baada ya kuona kwamba waandamanaji wameanza kutumia silaha za moto.

Johnson amesema kwamba askari polisi wanne wamejeruhiwa kwa mawe yaliyorushwa na waandamanaji, huku akibaini kwamba baadhi ya waandamanaji 200 ambao wamekua wakirusha mawe ni kutoka jimbo la New York na California.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.