Pata taarifa kuu
CANADA-Usalama

Canada: mashambulizi katika mji wa Ottawa

Michael Zehaf-Bibeau, mwenye umri wa miaka 32 aliuawa Jumatano Oktoba 22 na vikosi vya usalama wakati alipokua akijaribu kuingia ndani ya jengo la Bunge mjini Ottawa nchini Canada akiwa na silaha.

Wanajeshi wa Canada wakipiga doria karibu na jengo la Bunge mjini Ottawa, Jumatano Oktoba 22.
Wanajeshi wa Canada wakipiga doria karibu na jengo la Bunge mjini Ottawa, Jumatano Oktoba 22. REUTERS/Chris Wattie
Matangazo ya kibiashara

Hali hiyo ilizua wasiwasi, baada ya kusikika milio mingi ya risase ndani ya jengo hilo na kusababisha kifo cha mwanajeshi mmoja.

Inasadikiwa kua mtu huyo ana uhusiano na Martin Rouleau, aliye endesha shambulio Jumatano Oktoba 20 dhidi ya wanajeshi wawili mjini Québec. Hakuna kundi ambalo limedai kutekeleza mashambulizi hayo. Lakini viongozi wa Canada wana amini kwamba ni mashambulizi ya kigaidi.

Waziri mkuu wa Canada, Stephen Harper, amesema kuwa vitendo hivyo viliyotokea katika ardhi ya Canada Jumatatu na Jumatano wiki hii ni vitendo vya kigaidi.

Mashambulizi hayo yanatokea wakati ambapo Canada iliwatuma wanajeshi wake kushiriki katika muungano unaoongozwa na Marekani dhidi ya kundi la wapiganaji wa Dola la Kiislam.

Hata hivo, Stephen Harper, amesema Canada haitishiki na vitisho hivyo, na itaendelea na vita dhidi ya ugaidi hususan Kundi la wapiganaji wa Dola la Kiislam.

Michael Zehaf-Bibeau, ni mkaazi wa Montréal, na amekua akifahamika na vyombo vya sheria kutokana na uhalifu aliyokua akitekeleza katika miji ya Québec na Vancouver,

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.