MAREKANI-BALTIMORE-SHERIA-HAKI
Marekani : maafisa 6 wafunguliwa mashtaka Baltimore
Mahakama mjini Baltimore nchini Marekani imewafungulia mashtaka maafisa sita wa polisi kwa tuhma za kuhusika na kifo cha kijana mweusi Freddie Gray.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kiongozi wa mashtaka Marilyn Mosby amesema polisi hao wana kesi ya kujibu.
Gray alijeruhiwa akiwa kizuizini na baadae kupoteza maisha mwezi Aprili.
Kifo cha kijana huyo mweusi kilisabbaisha maaandamano makubwa katika miji mbalimbali nchini Marekani.
Freddie Gray alifariki kutokana na majeraha akiwa mikononi mwa polisi.
Awali maelfu ya watu waliandamana katika miji mikubwa nchini Marekani kushinikiza polisi kuacha kuwanyanyasa watu wenye asili ya Afrika.