CHINA - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumatatu 20 agosti 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Jumatatu 20 agosti 2012

Mke wa mwanasiasa maarufu nchini China ahukumiwa kifo

Gu Kailai akiwa mbelew ya mahakama
REUTERS/CCTV

Na Victor Robert Wile

Gu Kailai mke wa mwanasiasa maarufu nchini China Bo Xilai amehukumiwa kifo cha kumuua mfanyibiashara raia wa Uingereza Neil Heywood mwaka uliopita.

Wakati wa hukumu hiyo, Gu Kailai alisalia kimya huku akisomewa mashtaka ya kumuua mfanyibiashara huyo kwa kumpa sumu .

Hukumu aliyopata inaaminisha kuwa atasalia gerezani maisha yake yote,huku mshirika wake Zhang Xiaojun walioshirikiana kumuua mfanyibiashara huyo akihukumiwa kifungo cha miaka 9.

Kabla ya hukumu hiyo kutolewa Gu alikiri kumpa sumu mfanyibiashara huyo katika hoteli moja mjini Chongqing.

Aliongeza kuwa aliamua kuchukua uamauzi huo baada ya Heywood kumtisha mwanae wa kiume kuhusu makubaliano ya umiliki wa mali.
 

tags: China
MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close