Pata taarifa kuu
KOREA KASKAZINI-MAUAJI-SIASA

Korea Kusini : waziri wa Ulinzi anyongwa

Kiongozi wa Korea Kusini Kim Jong-un alimuua kwa risai waziri wake wa ulinzi kwa ajili ya uhaini na kutomuheshimu, imesema leo Jumatano asubuhi Idara ya ujasusi ya Korea Kusini. Waziri huyo wa ulinzi amliuawa hadharani kwa silaha nzito.

Kim Jong-un na majenerali wake, katika mazoezi ya kijeshi, picha ya zamani iliyowekwa wazi Februari 21 mwaka 2015.
Kim Jong-un na majenerali wake, katika mazoezi ya kijeshi, picha ya zamani iliyowekwa wazi Februari 21 mwaka 2015. REUTERS/KCNA
Matangazo ya kibiashara

Tangu kifo cha baba yake Kim Jong-il na kuingia kwake madarakani mwaka 2011, Kiongozi huyo kijana wa Pyongyang amekua akiwakunyonga baadhi ya washirika wake vigogo.

Visa vya kunyongwa kwa washirika vigogo wa kiongozi wa Korea Kaskazini vimeendelea kushuhudiwa tangu kiongozi huyo alipochukua madaraka baada ya kifo cha babake.

Kwa mujibu wa maafisa wa Upelelezi nchini Korea Kusini, waziri wa ulinzi wa Korea Kusini, Hyon Yong-Chol, aliuawa mwishoni mwa mwezi Aprili mbele ya mamia ya viongozi vigogo wa Korea Kaskazini kwa kutumia bunduki inayodungua ndege ya kivita.

Waziri huo wa ulinzi aliteuliwa kwenye wadhifa huo mwaka mmoja uliyopita, na alituhumiwa na Kim Jong-un wa kukaidi amri zake katika maadhimisho ya kijeshi, na kutofuata maelekezo ya yake.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.