SYRIA - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumamosi 26 mei 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Jumamosi 26 mei 2012

Watu 70 wauwawa nchini Syria siku chache kabla ya ziara ya Kofi Annan nchini humo

Mjumbe wa Umoja wa mataifa na jumuiya ya nchi za kiarabu katika mgogoro wa Syria Kofi Annan.
Mjumbe wa Umoja wa mataifa na jumuiya ya nchi za kiarabu katika mgogoro wa Syria Kofi Annan.
REUTERS/Tiksa Negeri

Na Sabina Chrispine Nabigambo

Zaidi ya watu 70 wameuwawa nchini Syria jana Ijumaa,wakati makumi ya maelfu ya waandamanaji wakiandamana mitaani huku mizinga ikitumika kuwatawanya waandamanaji katika mji wa Damascus, waangalizi nchini humo wamesema.

Machafuko hayo mapya yametokea wakati mjumbe wa umoja wa mataifa na jumuiya ya nchi za Kiarabu Kofi Annan ambaye anaongoza mpango wa kusitisha mapigano nchini humo akikamilisha mpango wa kurejea Damascus.

Wanadiplomasia mjini Geneva wamesema kuwa katibu mkuu huyo wa zamani wa Umoja wa mataifa anataraji kuzuru mji mkuu wa Syria mapema wiki ijayo.

Kofi Annan amekuwa akiongoza mpango wa kumaliza machafuko na umwagaji damu nchini Syria, mpango ambao hata hivyo umekuwa ukivunjwa mara kadhaa.
 

tags: Kofi Annan - Syria - Umoja wa Falme za Kiarabu
MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close