DR CONGO - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumapili 27 mei 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Jumapili 27 mei 2012

Jeshi la CONGO DR kupambana na waasi mashariki mwa Kivu

Wapiganaji waasi wa jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo
Wapiganaji waasi wa jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo
nyenyerinews.org

Na Martha Saranga Amini

Jeshi la serikali ya jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo limeendelea kupambana na waasi baada ya hali kuwa tete huko mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo baada ya mashambulizi ya mabomu hivi karibuni katika eneo la mipaka ya rwanda na uganda.

Jeshi hilo limekiri kukutana na upinzani mkali kutoka kwa waasi hao ambao wamekuwa wakijibu mashambulizi ya hatari.

Majeshi ya waasi nchini jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo yamejigamba jumamosi kuwa wamefanikiwa kujibu mashambulizi makali yaliyofanywa na majeshi ya serikali ya nchi hiyo huko mashariki mwa jimbo la Kivu.

Luteni kanali Vianney Kazarama, ambaye ni msemaji wa waasi alisema kuwa majeshi ya serikali yalitumia silaha kali wakijaribu kudhibiti eneo la Mbuzi na kushindwa baada ya kushambuliwa na kundi la waasi.

tags: Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close