Israel-Palestina - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Thursday 07 juni 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Thursday 07 juni 2012

Isreal kuendelea kujenga makaazi mapya katika ukingo wa Magharibi

Makaazi katika ukingo wa Magharibi

Na Victor Melkizedeck Abuso

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ametangaza kuwa serikali yake itajenga mamia ya makaazi ya walowezi katika ukingo wa Magharibi.

Tangazo la Netanyahu linakuja siku moja baada ya bunge la Israel kupitisha mswada wa kutaka serikali kutoendelea kujenga maakazi kwa sababu ya kisheria.

Netanyahu ameongeza kuwa serikali yake haitaruhusu tofauti za kisheria kuathiri ujenzi wa makaazi mapya 300 katika ukingo huo wa Magharibi karibu na mji wa Ramallah katika ngome ya Palestina.

Rais wa Palestina Mahmoud Abbas amekashifu uamuzi wa Netanyahu na kusema kuwa ujenzi wa makaazi hayo mapya ,kutadhoofisha juhudi za kusaka amani kati yao na Israel.

Washington pia kupitia kwa msemaji wake wa wizara ya mambo ya nje Mark Tonner nayo imekashifu hatu hiyo ya Israel ikiongeza kuwa, Jerusalem inarudisha nyuma juhudi za kupata amani kati ya Waisraeli na Wapalestina.

Mazungumzo ya amani kati ya Israel na Palestina yalivunjika miaka mitatu iliyopita na Palestina imesema kuwa haijarejea katika meza ya mazungumzo hadi pale Israel itakapoacha kujenga makaazi mapya katika ukingo wa Magharibi na Mashariki mwa mji wa Jerusalem.

Israel inasema mazungumzo hayo yanastahili kurejelewa bila ya masharti yeyote, wakati Palestina ikiendelea kuishtumu Israel kunyakua ardhi yao mwaka 1967.
 

tags: Israeli - Marekani - Palestina
MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close