Jeshi la kimataifa la kupambana na makundi ya uasi Mashariki mwa Congo kuwa na askari 4,000

Jeshi la kimataifa linalobuniwa kwa lengo la kusaidia kurejesha amani mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,linatarajiwa kuwa na askari 4,000 kutoka nchi mbalimbali za Afrika, Waziri wa Ulinzi Alexandre Luba Ntambo amesema jana Ijumaa.
Jeshi hilo la kimataifa lisilofungamana na upande wowote halitajumuisha askari kutoka DR Congo wala nchi yoyote katika zile zinazotuhumiwa kuhusika katika mapigano katika jimbo la Kivu amesema waziri Ntambo, siku sita baada ya kukutana na mawaziri wengine wa ulinzi kutoka katika ukanda huo wa maziwa makuu, kukabiliana na machafuko.
Nchi ambazo hadi sasa zinatajwa kuhusika katika mapigano Mashariki mwa Congo ni pamoja na DRC, Rwanda, Burundi na Uganda, hivyo kujumuishwa kwazo katika jeshi hilo si sahihi amesema waziri Ntambo.







MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya