cote d'Ivoire - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumapili 19 agosti 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Jumapili 19 agosti 2012

Waziri wa zamani Cote D' Ivoire ashikiliwa na wanausalama

Waziri wa zamani nchini Cote D'Ivoire,Alphonse Douat ambaye anashaikiliwa na wanausalama nchini humo.
Waziri wa zamani nchini Cote D'Ivoire,Alphonse Douat ambaye anashaikiliwa na wanausalama nchini humo.
news.abidjan.net

Na Martha Saranga Amini

Vyombo vya usalama nchini Cote d' Ivoire vimemuweka kizuizini waziri wa zamani nchini humo Alphonse Douati,mtu muhimu katika chama cha raisi wa zamani Laurent Gbagbo ikiwa ni masaa machache baada ya shambulizi kutokea katika ofisi za chama cha IPF.

Msemaji wa vyombo vya usalama nchini humo Mamadou Frank Bamba amethibitisha kwamba Douati,ambaye kwa sasa ni kaimu katibu mkuu wa chama cha IPF ameshikiliwa na wanausalama kwa mahojiano zaidi ambapo zoezi hilo litafanyika katika ofisi za usalama nchini humo.

Hata hivyo sababu hasa ya kumuweka kizuizini kiongozi huyo wa IPF haijawekwa wazi.

Hayo yanajiri kufuatia kushambuliwa kwa Makao makuu ya chama cha raisi wa zamani wa Cote d' Ivoire Laurent Gbagbo na kundi la watu wenye silaha na kujeruhi watu watatu huku wawili wakitoroshwa,na kushuhudia lawama zikielekezwa kwa wafuasi wa raisi Ouattara.

tags: Alassane Ouattara - Côte d’Ivoire - Laurent Gbagbo
MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close