Pata taarifa kuu
UGANDA

Mkutano wa viongozi wa nchi za maziwa makuu (ICGLR) wamalizika bila ufumbuzi wa amani Mashariki mwa DRC

Mkutano wa viongozi wa nchi za maziwa makuu kuhusu hali ya usalama mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo umemalizika hapo jana jijini Kampala nchini Uganda huku kukiwa hakuna ufumbuzi wa kudumu katika machafuko sugu mashariki mwa nchi hiyo. 

presstv.com
Matangazo ya kibiashara

Viongozi chini ya theluthi moja walioalikwa wamehudhuria mkutano huo jijini Kampala,chini ya mwenyeji rais Yoweri Museven, jambo linaloashiria kuwa suala la kuundwa kwa jeshi huru lisilofungamana na upande wowote kutatua mzozo huo wa Congo bado litaendelea kuwa kitendawili.

Katika taarifa kufuatia mkutano wa Jumamosi, viongozi hao wa maziwa makuu wamesema kuwa iwapo jeshi hilo litaundwa litapelekwa nchini DRC kwa mamlaka ya Umoja wa Afrika na Umoja wa mataifa.

Viongozi hao pia wametoa wito kwa mawaziri wa ulinzi wa ukanda huo kuharakisha utendaji kuelekea kuanza kazi kwa jeshi huru la kimataifa ndani ya miezi mitatu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.