MISRI - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumamosi 26 mei 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Jumamosi 26 mei 2012

Chama cha udugu wa kiislam chawaomba wamisri kumuunga mkono mgombea wake katika duru la pili la uchaguzi.

Wagombea wa urais nchini Misri
Wagombea wa urais nchini Misri
viewtz.com

Na Sabina Chrispine Nabigambo

Chama cha udugu wa kiislam cha nchini Misri, Muslim Brotherhood, kimewataka Wamisri kumuunga mkono mgombea wao wa urais katika duru la pili la uchaguzi dhidi ya mpinzani wake Ahmed Shafiq, kikionya kwamba nchi itakuwa hatarini endapo aliyekuwa waziri mkuu katika kipindi cha utawala wa kiimla wa rais Hosni Mubarak atashinda.

Chama cha Muslim brotherhood jana Ijumaa kilitangaza kuwa mgombea wake Mohammed Mursi anaongoza katika uchaguzi uliofanywa May 23 na 24 baada ya kura zote kuhesabiwa huku mpinzani wake Ahmed Shafiq akifuatia katika nafasi ya pili.

Hatua ya kurudiwa kwa uchaguzi kati ya Shafiq na Mursi itazidi kuligawa taifa hilo ambalo raia wake walisimama kupinga utawala wa mabavu wa rais Hosni Mubarak miezi 15 iliyopita lakini tangu wakati huo linakabiliwa na vurugu na kushuka kwa uchumi.

Tume ya uchaguzi inatarajiwa kutangaza matokeo rasmi siku ya Jumanne.

tags: Hosni Mubarak - Misri
MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close