SYRIA -
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumamosi 09 juni 2012 -
Taarifa za ivi karibuni : Jumamosi 09 juni 2012
Waangalizi wa umoja wa mataifa washuhudia damu na harufu ya miili iliyochomwa moto kijijini Al Kubeir

Msemaji wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa UN Martin Nesirky
unmultimedia.org
Waangalizi wa Umoja wa Mataifa ambao walikwenda katika kijiji cha Al-Kubeir yalikotokea mauaji ya kinyama nchini Syria wamesema wameona damu juu ya kuta na wakahisi harufu ya mwili kuteketezwa lakini hawakuweza kuthibitisha idadi ya waliouwawa.
Wakati serikali ikikanusha kuhusika na mauaji hayo,msemaji wa Umoja wa Mataifa Martin Nesirky amesema kuwa waangalizi wameshuhudia magari ya kivita katika maeneo ya kijiji hicho, nyumba zilizoharibiwa na makombora, mabomu na silaha mbalimbali.
Takribani watu 55 waliuawa siku ya Jumatano katika shambulizi kijijini Al-Kubeir katika jimbo la Hama, kwa mujibu wa taasisi ya waangalizi wa haki za binadamu ya nchini Syria.







MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya