Yemeni - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumatatu 21 mei 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Jumatatu 21 mei 2012

Watu wasiopungua 96 wauawa nchi Yemeni

Hali ya mambo nchini Yemeni katika picha
RFI

Na Victor Robert Wile

Watu wasiopungua 96 wameuawa kutokana na shambulio la bomu la kujitoa mhanga lililotokea katika mji mkuu wa Sanaa nchini Yemeni wamesema maafisa wa Serikali.

Shambulio hilo la bomu limetokea katika eneo ambalo wanajeshi walikua wakifanya mazoezi ya gwaride ambapo mtu aliyefanya shambulizi hilo alikua amevaa nguo za kijeshi alijilipua katika kundi la wanajeshi katika uwanja wa al-Sabin Square karibu na Ikulu ya Rais.

Shambulio linaelezewa kuwa ni kubwa kuwahi kutokea tangu rais Abdrabbuh Mansour Hadi, aingie madarakani mwezi Februari kufuatia wimbi la vuguvugu la kisiasa katika nchi za kiarabu.

Kundi la kigaidi la Al Qaeda limetangaza wazi kwamba limehusika na shambulio hilo ambalo limesababisha vifo hivyo huku wanaume wengi wakiangamia baada ya mtu huyo kujilipua.

Kundi la Al Qaeda limekuwa likilaumiwa kwa kuhatarisha usalama wa dunia kwa kufanya mashambulizi katika maeneo mbalimbali duniani na shambulio hilo linaashiria kuwa bado Yemeni inakabiliwa tishio la usalama na mauaji.

tags: Al Qaeda - Sanaa - Siasa - Yemeni
MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close