Pata taarifa kuu
ISRAEL-PALESTINA-UGAIDI

Israel: "hakuna kuwavumilia Wayahudi wenye msimamo mkali"

Israel imesema haitowavumilia Wayahudi wenye msimamo mkali ambao wamekua wakijihusisha na vitendo viovu dhidi ya raia wa palestina.

Muhusika wa mashambulizi dhidi ya washiriki wa Gay Pride jijini Jerusalem akipokonywa silaha na polisi. Mmoja wa waathirika wa shambulio hilo  amefariki dunia Jumapili Agosti 2.
Muhusika wa mashambulizi dhidi ya washiriki wa Gay Pride jijini Jerusalem akipokonywa silaha na polisi. Mmoja wa waathirika wa shambulio hilo amefariki dunia Jumapili Agosti 2. REUTERS/Amir Cohen
Matangazo ya kibiashara

Uamzi huo unakuja baada ya kijana mmoja kuchomwa kisu na Myahudi mmoja mwenye msimamo mkali wakati wa sherehe ya mashoga jijini Jerusalem Alhamisi juma lililopita, Kijana huyo amefariki Jumapili mwishoni mwa juma hili lililopita.

Baada ya machafuko yaliyotokea siku za hivi karibuni, serikali ya Israel imechukua hatua dhidi ya Wayahudi wenye msimamo mkali.

Baraza la usalama la kitaifa nchini Israel limekutana Jumapili Agosti 2 ili kutathmini athari za shambulio lililotokea katika kijiji cha Douma, kaskazini mwa Cisjordania, na lile llililoptokea wakati wa sherehe ya mashoga jijini Jerusalem. Mawaziri wametoa idhni kwa vikosi vya usalama ili wachukuwe hatua zinazohitajika kwa kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria wahusika wa mashambulizi hayo.

Shambulio la kigaidi

Aina hii ya kukamatwa itatekelezwa baada ya kupitishwa na mshauri wa serikali anayehusika na maswala ya sheria ambaye atajadiliana na Mwendesha mashtaka mkuu wa jamhuri. Israel imelaani pia shambulio lililosababisha kifo cha mtoto mchanga Ali Dawabcheh. Israel imetaja shambulio hilo kuwa ni la kigaidi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.