SERIA A - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumatano 09 mei 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Jumatano 09 mei 2012

Shirikisho la soka nchini Italia laanzisha uchunguzi dhidi ya vilabu 20 vinavyotuhumiwa kupanga matokeo

Mashabiki wa soka nchini Italia wakiingia uwanjani mara baada ya mchezo
Mashabiki wa soka nchini Italia wakiingia uwanjani mara baada ya mchezo
Reuters

Na Emmanuel Richard Makundi

Chama cha soka nchini Italia kimetangaza kuanzisha uchunguzi dhidi ya timu zaidi ya 20 kwa tuhuma za kuhusika na njama za upangaji matokeo.

Shirikisho la mpira nchini humo limesema kuwa zaidi ya wati 61 watahojiwa wakiwemo wachezaji 52 wa vilabu mbalimbali nchini ambao wanatuhumiwa kuhusika na njama za kupanga matokeo kwenye mechi zao.

Katika ripoti ya shirikisho hilo imesema kuwa tayati watu zaidi ya 30 wamekamatwa na polisi kwa mahojiano kuhusiana na kupanga matokeo kwenye mechi za ligi daraja la kwanza nchini humo.

Uchunguzi huu mpya unakuja wakati ambapo itakumbukwa msimu wa mwaka 2006 timu ya Juventus iliyokuwa kwenye Seria A ilishushwa daraja baada ya kubainika kupanga matokeo.

Ofisi ya mwendesha mashtaka nchini humo imesema kuwa maofisa wake wanachunguza zaidi ya mechi 33 ambazo matokeo yake yanaelezwa kuwa na utata kutokana na baadhi ya timu kuhonga ili kupata ushindi kwenye mechi zao.

 

tags: Italia - Ligu Kuu Nchini Italia - SERIA A
MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close