TENNIS-FRENCH OPEN - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Ijumaa 08 juni 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Ijumaa 08 juni 2012

Maria Sharapova na Sara Errani kumenyana katika fainali ya French Open siku ya Jumamosi

Maria Sharapova

Na Victor Melkizedeck Abuso

Maria Sharapova kutoka Urusi na Sara Errani kutoka Italia watamenyana katika fainali ya makala ya mwaka huu ya mashindano ya Tennis ya French Open kwa upande wa akina dada  yanayoendelea jijini Paris  Jumamosi hii .

Sharapova anayeorodheswa wa pili duniani alitinga fainali baada ya kumchabanga Petra Kvita kutoka Jamhuri ya Czech kwa seti 2 kwa 0 za  6-3 na 6-3, huku Errani anayeorodheshwa wa 21 akimshinda Samantha Stosur kutoka Australia  anayeshikilia nafasi ya  6  duniani kwa seti za 2 kwa 1 za 7-5, 1-6, 6-3.

Sharapova ambaye amewahi kushinda taji la Wimbledon mwaka 2004 huko Uingereza, US Open nchini Marekani mwaka 2006 na 2008 anapewa nafasi kubwa ya kunyakua taji hilo dhidi ya Errani ambaye anafikia katika fainali ya michunao mikubwa kama hii kwa mara ya kwanza.

Ikiwa Sharapova ataibuka mshindi ataorodheswa katika nafasi ya kwanza kama mwanamke bora duniani na kuchukua nafasi ya Li Na kutoka nchini China aliyeshinda michuano hii mwaka uliopita na kuondolewa mapema katika kinganyiro hiki.

Kwingineko, kwa upande wa wanaume katika nausu fainali Ijumaa, Mserbia Novak Djokovic anachuana na Mswizi Roger Federer wakati David Ferrer akimaliza kazi na Rafael Nadal.

Fainali ya wanaume itachezwa Jumapili hii.

MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close