POLAND-EURO 2012 - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Ijumaa 08 juni 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Ijumaa 08 juni 2012

Mashindano ya soka ya bara la Ulaya kuanza nchini Poland na Ukraine

Uwanja wa soka nchini Poland

Na Victor Melkizedeck Abuso

Makala ya mwaka 2012 ya soka ya kutafuta bingwa wa bara la Ulaya yaaanza Ijumaa usiku nchini Poland.

Wenyeji Poland wanafungua dimba dhidi ya Ugiriki katika uwanja wa taifa wa Warsaw katika mashindano hayo yanayoyakutanisha mataifa 16.

Poland watakuwa wanacheza mechi yao ya ufunguzi mbele ya mashabiki wa nyumbani wakisaka ushindi , huku Ugiriki nao ambao wamekuwa wakikabiliana na hali ngumu ya kiuchumi wakitaka kuwadhirishia wapenzi wa soka kuwa wao ni moto wa kuotea mbali.

Poland imejumuishwa katika kundi moja na Urusi na Jahmuri ya Czech ,kipute ambacho Uhispiania ambao ni mabingwa watetezi wanasema wanataka kunyakua tena ubingwa huo baada ya kuishinda Ujerumani mwaka 2008.

Haya ndio mashindano ya kwanza kuandaliwa na mataifa mawili ambapo Ukraine watafungua mchuano wao dhidi ya Sweden siku ya Jumatatu juma lijalo na wamejumuishwa katika kundi moja na Ufaransa na Uingereza.

Suala la ubaguzi wa rangi katika mashindano haya linaedelea kuzungumziwa na kuzua mjadala mkubwa, baada ya maafisa wa timu ya taifa ya Uholanzi kuripoti visa vya ubaguzi wa rangi kwa kile wanachosema wachezaji wao wameimbiwa nyimbo za kuwabagua na mashabiki wa soka nchini Poland.

Maafisa wa soka wa Uholanzi wanasema wamewafahamisha viongozi wa shirikisho la soka barani Ulaya, UEFA kuhusu tukio hilo.

MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close