Simba B yaibuka kidume,yaibamiza Mtibwa sugar 4-3

Kikosi cha pili cha timu ya Simba kimeonesha umwaba baada ya kuutwaa ubingwa wa michuano ya kwanza ya Banc ABC SUP8R kwa kuilaza Mtibwa sugar kwa mabao 4 kwa 3 katika mchezo uliofanyika kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam nchini Tanzania.
Dakika 120 za mchezo zilimalizika kwa matokeo hayo baada ya kushuhudia Edward Christopher kuanza kuifungulia Simba bao la awali katika dakika ya 12 baada ya kumshangaza kipa wa Mtibwa langoni mwake,huku goli lingine likizamishwa kimiani dakika ya 32 ambapo Mtibwa sugar ilisawazisha bao la awali.
Kwa ushindi huo,Simba imejinyakulia kitita cha milioni 40 pamoja na medali,sambamba na mchezaji wale Edward Christopher akizawadiwa milioni mbili kwa kuwa mfungaji bora huku Mtibwa ikiondoka na milioni 20 pamoja na medali.







MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya