UHISPANIA - 
Makala iliyochapishwa tarehe : Jumatatu 17 septemba 2012 - Taarifa za ivi karibuni : Jumatatu 17 septemba 2012

Mourinho achukizwa na mlolongo wa matokeo mabaya ya Real Madrid kwenye La Liga msimu huu

Kocha wa Real Madrid Jose Mourinho akiwa anafuatilia mchezo kwa makini lakini amekiri kuchukizwa na mwenendo wa Klabu yake
Kocha wa Real Madrid Jose Mourinho akiwa anafuatilia mchezo kwa makini lakini amekiri kuchukizwa na mwenendo wa Klabu yake
© Reuters

Na Nurdin Selemani Ramadhani

Kocha Mkuu wa Real Madrid Jose Mourinho amechukizwa na mwenenendo mbaya wa Timu yake kwenye Ligii nchini Uhispania mwaka huu kutokana na kuwa na matoke mabaya yakichangiwa na kufungwa na Sevilla.

Mourinho amehoji uwezo na morali ya wachezaji wake kutokana na kucheza michezo minne ya ligi na kuambulia pointi nne pekee kitu ambacho kimeanza kuzua maswali kama Real Madrid itaweza kutetea ubingwa wake.

Mourinho ameonekana kutokuwa na raha kabisa baada ya kushuhudia wakipoteza michezo miwili kwenye ligi ya msimu huu wakati mahasimu wao Barcelona wakiendelea kuchanja mbunga kwa kushinda michezo yao yote minne.

Kocha huyo mwenye maneno mengi na anatambulika kwa jina la Special One amekitaka kikosi chake kubadilika na kuhakikisha wanapata ushindi kwenye mchezo wa kwanza wa makundi wa Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya dhidi ya Manchester City.

Mourinho amewaambia wanahabari timu yake haichezi vizuri kabisa kitu ambacho kinampa wasiwasi ya kwamba msimu huu hana kikosi imara cha kupambana na kushinda mataji licha ya kuanza kwa kushinda Super Cup.

Kocha huyo Mreno ameongeza kama timu haina wachezaji ambao wanajitolea inakuwa vigumu kuweza kupata ushindi na kutimiza malengo ya kutwaa mataji mengi kama ambavyo wengi wamekuwa wakifikiri.

Mourinho hakuacha kuisifia Sevilla kwa ushindi ambao wameupata na kuweka bayana bila ya wasiwasi yoyote walistahili kushinda kutokana na kuonesha mchezo mzuri dhidi ya Real Madrid.

Kocha huyo wa zamani wa Chelsea amekataa kata kata kushusha lawama zake kwa Cristiano Ronaldo akiamini kile ambacho kimetokea ni suala la kawaida kwa mchezaji yoyote.

tags: Cristiano Ronaldo - Jose Mourinho - Manchester City - Real Madrid FC - Sevilla
MAELEZO
Tuma maoni yako kwa makala haya
Maudhui ya eneo hili yatakuwa ya kibinafsi na kuto kuonyeshwa kwa watu wote.
To prevent automated spam submissions leave this field empty.
CAPTCHA
Swali hili ni kwa ajili ya kupima kama wewe si roboti ili kuzuia spam ya papo kwa papo.
Close