Pata taarifa kuu
BOSTON-Riadha

Boston: Mamia ya wanariadha wajitokeza kushiriki mbio za marathon

Takriban watu milioni moja na wanariadha elfu 35, wanasubiriwa leo jijini Boston nchini Marekani kuadhimisha mbio za Marathon ikiwa ni mwaka mmoja tangu kutokea kwa mlipuko wa bomu uliogharimu maisha ya watu watatu, na ambapo mwaka huu polisi imetanda katika kila kona kuhakikisha usalama umaimarika.

Mripuko wa bomu uliyotokea mjini Boston wakati wa mbio za marathon aprili mwaka 2013.
Mripuko wa bomu uliyotokea mjini Boston wakati wa mbio za marathon aprili mwaka 2013. REUTERS/Dan Lampariello
Matangazo ya kibiashara

Polisi wapatao elfu tatu na mia tano wametawanywa katika mji mkuu wa Massachusetts kaskazini mashariki mwa Marekani ikiwa ni mara mbili ya idadi iliokuwa mwaka uliopita, zaidi ya hao walinzi wa kikosi cha taifa wapata 600 na wengine walinzi 3.500 wa kampuni binafsi.

Kamati ya maandalizi ya mbio hizo imedhamiria usalama vya kutosha wakati huu idadi pia ya wanariadha ikiongezeka, ukilinganisha na mwaka uliopita. Mbio hizo zliingia dosari mwaka jana pale vijana wawili wa kiislam wenye asili ya ki tchetcheni walitega bomu ndani ya begi lililolipuka na kugharimu maisha ya watu watatu.

Kamati ya maandalizi imechukua hatua zinazohakikisha kuwa usalama umeimarishwa ipasavyo, huku mifuko yoyote ikipigwa marufuku, na kuamrisha watakaohudhuruia mbiyo hizo iwapo watapendelea kutumia mifuko ya kuhifadhi nguo zao watumiye mifuko inayoonshesha kilicho ndani.

Askari polisi ikizidisha ulinzi, baada ya mlipuko wa bomu wakati wa mbio za marathon, aprili 19 mwaka 2013..
Askari polisi ikizidisha ulinzi, baada ya mlipuko wa bomu wakati wa mbio za marathon, aprili 19 mwaka 2013.. REUTERS/Brian Snyder

Bomu liliyolipuka mwaka jana liliwekwa ndani ya mfuko unaobebwa mgongoni na baadae uliwekwa kwenye aridhi na ndugu wawili kutoka jamii ya waislamu raia wa Checheniya.

“Tuko makaini , na tumejiandalia vizuri. Tunawapa matumaini watu wanaoshiriki na wale wanaohudhuria mbio hizi kwamba leo ni sikukuu kubwa, na siku ya matumaini”, mkuu wa jimbo la Deval Patrick, ameelezea jana jumapili, kituocha habari cha CBS.

Kwa mujibu wa kamati ya maadalizi, zaidi ya wanahabari 1800 wamejielekeza mjini Boston kuhudhuria mbio hizo.

Vijana waliyohusika katika shambulio la bomu mjini Boston, mmoja, ambaye anajulikana kwa jina la Djokhar, mwenye umri wa miaka 19 yu hai na mwengine, Tamerlan Tsarnaev, mwenye umri wa miaka 26 aliuawa na polisi alipokua akijaribu kujificha, aprili 19 mwaka jana. Picha ya mtuhumiwa huyo aliyeuawa hii hapa.

Mshukiwa wa shambulio la bomu wakati wa mbio za marathon mjini Boston (kulia akivalia miwani), aliuawa akijaribu kujificha, huyu wa kofia nyeupe (kushoto) bado anatafutwa.
Mshukiwa wa shambulio la bomu wakati wa mbio za marathon mjini Boston (kulia akivalia miwani), aliuawa akijaribu kujificha, huyu wa kofia nyeupe (kushoto) bado anatafutwa. Reuters/FBI

Djokhar, anakabiliwa na adhabu ya kifo, na hukumu yake itatolewa novemba 3 mwaka huu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.