Pata taarifa kuu
AFRIKA-SOKA-MICHEZO-CAN 2015

Nigeria: Meneja wa timu ya taifa ya Nigeria afutwa kazi

Shirikisho la soka nchini Nigeria limemfuta kazi, kocha wa timu ya taifa Stephen Keshi licha ya ushindi wa Super Eagles dhidi ya Sudan.

Kocha wa timu ya taifa ya  Nigeria, Stephen Keshi baada ya ushindi wa timu yake, Februari 10 mwaka 2013.
Kocha wa timu ya taifa ya Nigeria, Stephen Keshi baada ya ushindi wa timu yake, Februari 10 mwaka 2013. EUTERS/Siphiwe Sibeko
Matangazo ya kibiashara

Nigeria imeibwagiza Sudan mabao 3 kwa 1 jana Jumatano jijini Abuja katika mchuano wa kusakata tiketi ya kufuzu kwa michuano ya kuwania ubingwa wa Afrika mwaka ujao nchini Morroco mwaka ujao.

Kocha wa zamani Shuaibu Amodu amepewa kazi ya kuifunza Nigeria kwa muda mfupi kabla ya kuajiriwa kwa kocha mwingine kutoka nchi ya kigeni.

Amodu ataingoza Nigeria katika michuano inayosalia ya kutafuta tiketi ya kwenda Morroco baada ya ushindi wa Jumatano wiki hii, ambapo Super Eagles wanahitaji kushinda mechi zinazosalia.

Kwa sasa Nigeria wana alama nne katika kundi la A, na ushindi wa jana ulikuwa wa kwanza tangu kuanza kwa kampeni hii.

Wachambuzi wa soka wanasema ilitarajiwa Keshi kufutwa kazi baada ya kuingoza Nigeria katika kombe la dunia nchini Brazil mwaka huu, na pia kuisaidia Super Eagles kunyakua taji la Afrika mwaka jana, na kutofanya vizuri katika michuano ya kwenda Morroco.

Viongozi wa kandanda nchini Nigeria wamesema wamechukua hatua hiyo kwa maslahi ya mchezo huo nchini humo, na kumpa Keshi nafasi ya kumpumzika baada ya kuisaidia Super Eagles.

Stephen Keshi, meneja wa timu ya taifa ya Nigeria ambaye amefutwa kazi.
Stephen Keshi, meneja wa timu ya taifa ya Nigeria ambaye amefutwa kazi. Reuters/Thomas Mukoya

Keshi mwenye umri wa miaka 52 aliteulwia kuifunza Super Eagles mwaka 2011, na pia aliwahi kuwa kocha wa timu ya taifa ya Togo na Mali kati ya mwaka 2004 na 2011.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.