Pata taarifa kuu
KENYA LEOPARS-SOKA

AFC Leopards mbioni kuwakosa wachezaji wake 10

Mabingwa wa zamani wa soka ligi kuu nchini Kenya AFC Leopards wanapanga kuachana na wachezaji 10 wakati wa kipindi cha dirisha dogo la kuwasajili wachezaji mwezi ujao.

Timu ya taifa ya soka ya Kenya, Harambee Stars.
Timu ya taifa ya soka ya Kenya, Harambee Stars. youtube
Matangazo ya kibiashara

Kocha Ivan Minnaert anatarajiwa kutumia nafasi hiyo kuwatafuta wachezaji watakaoisadia klabu hiyo kunyakua ubingwa wa ligi kuu msimu huu.

Miongoni mwa wachezaji wanatarajiwa kuondoka katika klabu hiyo ni pamoja na mabeki Israel Emuge, Erick Masika na Solomon Nasio. 

AFC Leopards ambayo mwisho ilishinda taji kuu la ligi kuu nchini Kenya mwaka 1998 ni ya tano kwa alama 18.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.