Pata taarifa kuu
KENYA-UGAIDI-USALAMA

Kenya: Waislam zaidi ya 150 watuhumiwa ugaidi

Jeshi la polisi nchini Kenya limesema kuwa litawafikisha mahakamani zaidi ya watu 150 kwa tuhuma za kushirikiana na kundi la kigaidi la Al Shabab. Operesheni polisi ya kuwasaka wafuasi wa kundi hilo inaendelea katika misikiti kadhaa inayodaiwa kutoa mafunzo ya itikadi kali za kidini katika mji wa Mombasa.

Wanajeshi wa Kenya wakijianda kukabiliana na watu waliovamia na kuteka jumba la kibiashara la Westgate mjini Nairobi, Sptemba 24 mwaka 2013.
Wanajeshi wa Kenya wakijianda kukabiliana na watu waliovamia na kuteka jumba la kibiashara la Westgate mjini Nairobi, Sptemba 24 mwaka 2013. REUTERS/Noor Khamis
Matangazo ya kibiashara

Katika operesheni ya polisi ya hivi karibuni katika Misikiti mbalimbali mji Mombasa, watu 250 walikamatwa wakituhumiwa kushirikiana na kundi la Al Shabab linaloendesha harakati zake nchini Somalia.

Watuhumiwa hao walifikishwa Mahakamani, lakini watuhumiwa 91 waliachiliwa huru kwa kukosekana ushahidi wa kutosha.

Hata hivyo watuhumiwa wengine zaidi ya 150 bado wanazuiliwa jela. Polisi nchini Kenya imesema itawafungulia mashtaka watuhumiwa hao kwa kosa la kushirikiana na kundi la Al Shabab.

Mashirika yanayotetea haki za binadamu nchini Kenya yamesema kwamba watu hao wanaozuiliwa jela hawana hatia yoyote, bali ni mbinu za utawala za kutaka kuendelea kuwakandamiza baadhi ya watu kutoka jamii ya Waislam.

Kenya imekua ikishuhudia mashambulizi ya mara kwa mara tangu rais Uhuru Kenyatta achukuwe hatamu ya uongozi wa nchi. Kundi la Al Shabab limekua likinyooshewa kidole kuhusika na mashambulizi hayo.

Viongozi tawala wamewataka raia kushirikiana na polisi ili kuwafichua wahalifu hususan watu wanaoshirikiana na makundi ya kigaidi kwa lengo la kuimarisha usalama wa taifa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.