Zaidi ya ishirini waangamia katika milipuko Equatorial Guinea
Watu zaidi ya 2O wamefariki katika milipuko mikubwa iliotokea katika kambi ya jeshi katika mji wa Bata, mji mkuu wa uchumi wa Equatorial Guinea.
Imechapishwa:
Zaidi ya watu 600 walijeruhiwa katika mlipuko huo uliotokea katika ghala la silaha, kulingana na ripoti rasmi ya awali.
Milipuko hiyo imesababishwa na "uzembe" uliohusishwa na hifadhi ya baruti kali kambini, rais wa Eguatorial Guinea amesema.
Rais Teodoro Obiang Nguema amesema katika taarifa kwamba athari iliyotokana na mlipuko huo "imesababisha uharibifu mkubwa wa mali na vitu huko Bata", na kutoa wito kwa jamii ya kimataifa kusaidia.
Katika mtandao wa Twitter, balozi wa Ufaransa Olivier Brochenin ametuma risala zake za rambi rambi kwa waathirika, akizungumzia ajali hiyo kama "janga".
Mi más sentido pésame por la catástrofe que acaba de producirse en Bata. Mis pensamientos están con todas las víctimas. Solidaridad. @AngueSimeon @MCooperacion pic.twitter.com/01dx7518i2
— Brochenin Olivier (@O_Brochenin) March 7, 2021
Waziri wa afya wa Equatorial Guinea ameomba wahudumu wa afya kujitolea na kwenda katika hospitali ya eneo la Bata. Pia imetoa wito watu kujitolea kutoa damu kwasababu ya idadi kubwa ya waliojeruhiwa.