Misri : Wanawake wawili wafariki baada ya kushambuliwa na Papa
Mamlaka nchini Misri, zimesema wanawake wawili wameuawa baada ya kushumbuliwa na samaki aina ya Papa, wakati wakiogelea katika bahari ya shamu.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Wizara ya mazingira nchini humo imesema vifo hivyo vilitokea umbali wa mitaa 600, raia wa Austria akifariki ijumaa kutokana na majiraha aliyopata baada ya kushambuliwa na papa.
Katika kisa kingine tofauti mwanamke mwenye umri wa miaka 40, raia wa Romania pia amefariki baada kushambuliwa na samaki aina ya papa.
Visa hiki vimeripotiwa katika eneo la Hurghada, eneo ambalo ni kivutio kikubwa cha watali nchini Misri, mamlaka zikilazimika kufunga baadhi ya maeneo kutokana visa hivyo viwili.