Sierra Leone: Polisi wamezingira makao makuu ya chama cha upinzani
Wanajeshi wamezingira makao makuu ya chama kikuu cha upinzani nchini Sierra Leone, huku kura zikihesabiwa katika uchaguzi wa urais uliofanyika nchini humo.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Mgombea mkuu wa upinzani Samura Kamara kupitia ukurasa wake wa Twitter, amedai kuwa risasi ilifwatuliwa ndani ya ofisi yake huku kukiwa na ripoti kuwa mwanamke mmoja alipoteza maisha.
They have tried it three times on our lives with my running mate. First @Mile38, second attempt was @Kono and now @apc_sl Headquarters pic.twitter.com/lcxFeXPK0d
— SamuraKamara2023 (@samurakamara201) June 25, 2023
Kiongozi huyo wa chama cha All People's Congress, Samura Kamara, amesema tukio hilo ni sawa na jaribio la mauaji.
Waangalizi wa Kimataifa wameonesha wasiwasi wao kuhusu muda mrefu unaotumiwa kujumuisha matokeo ya urais.
Haijabainika ni kwa nini wanajeshi ilitumwa katika eneo hilo, swala ambalo maofisa wa polisi bado hawajazungumzia.
I have been barricaded in my APC party headquarters during my live press conference. Live bullets and tear gassed fires at my offices by government forces. @USEmbFreetown @UKinSierraLeone @UN @_AfricanUnion
— SamuraKamara2023 (@samurakamara201) June 25, 2023
What is my country defending into. Is this an assignation attempt on… pic.twitter.com/fobnToKWpt
Upinzani nchini humo unatarajia kumuondoa madarakani rais Julius Maada Bio, ambaye anawania kwa muhula wa pili.
Kulikuwa na ghasia za hapa na pale dhidi ya maafisa wa uchaguzi wakati wa upigaji kura siku ya Jumamosi baada ya kampeni za mvutano.