Pata taarifa kuu
USALAMA-HAKI

Cameroon: RSF yaonya kuhusu waandishi wa habari katika maeneo yanayozungumza Kiingereza

Shirika la Waandishi wa Habari wasio na mipaka RSF limebaini vitisho ambavyo wakati mwingine kuwa vitendo. Taarifa hiyo inakuja wakati waandishi wa habari watatu wameuawa nchini humo tangu mwanzoni mwa 2023. Wa mwisho wao, Anye Nde Nsoh, aliuawa miezi minne iliyopita huko Bamenda, kaskazini-magharibi mwa nchi. Alikuwa na umri wa miaka 26 tu.

Askari wakipiga doria Bafut, Kaskazini-Magharibi mwa Cameroon, katika eneo linalozungumza Kiingereza, Novemba 15, 2017.
Askari wakipiga doria Bafut, Kaskazini-Magharibi mwa Cameroon, katika eneo linalozungumza Kiingereza, Novemba 15, 2017. AFP
Matangazo ya kibiashara

"Tumrekodi, mbali na mauaji ya mwandishi huyo wa habari, visa kadhaa vya utekaji nyara. Pia tumerekodi watu kadhaa kukamatwa kiholela na kuwekwa kizuizini. Hii pia inafichua kiwango ambacho waandishi wa habari na maripota katika maeneo haya wanafanya kazi kwa ukosefu wa usalama kwani wanalengwa na makundi ya waasi wanaotaka kujitenga na vikosi vya jeshi vya Cameroon. Na wanapaswa kuwa waangalifu kila wakati, na hata mara nyingi - tulizungumza na baadhi yao juu ya hili - hata wakati wanajaribu kuwa na wazi wakifanya kazi yao kwa uchunguzi zaidi, mara nyingi wanashutumiwa na vikosi vya usalama na ulinzi kwamba wao ndio wanatuma habari kwa makundi ya waasi wanaotaka kujitenga. Na kwa upande wao pia, makundi yenye silaha yanayotaka kujitenga yanawanyanyasa waandishi wa habari, hivyo ni muhimu kwa mamlaka katika ngazi ya kati kuweka mikakati madhubuti ya kuwalinda wanahabari ili kuepusha mikoa hii inayozungumza Kiingereza kuwa maeneo ya watu wasio na habari,” RSF imeonya katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.