Pata taarifa kuu

Blinken atamatisha ziara yake barani Afrika nchini Angola

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken anamalizia ziara yake barani Afrika nchini Angola siku ya Alhamisi yenye lengo la kudumisha ushawishi wa Washington katika bara ambalo China na Urusi zinazidi kuwepo.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken, kushoto, na Rais wa Angola Joao Lourenco wakipeana mkono wakati wa mkutano wao kwenye Ikulu ya rais mjini Luanda, Angola, Alhamisi, Jan. 25, 2024.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken, kushoto, na Rais wa Angola Joao Lourenco wakipeana mkono wakati wa mkutano wao kwenye Ikulu ya rais mjini Luanda, Angola, Alhamisi, Jan. 25, 2024. AP - Andrew Caballero-Reynolds
Matangazo ya kibiashara

 

Baada ya Nigeria, nchi yenye watu w na yenye wengi na yenye uchumi mkubwa zaidi barani Afrika, aliwasili siku ya Jumatano jioni huko Luanda, mji mkuu wa koloni hili la zamani la Ureno na mzalishaji mkubwa wa mafuta. Alikutana Alhamisi asubuhi na Rais Joao Lourenço, ambaye alikutana na Joe Biden katika Ikulu ya Marekani miezi miwili iliyopita, kabla ya kuondoka katika nchi hii ya kusini mwa Afrika mchana.

Nchi hizo mbili zimekuwa karibu zaidi katika miaka ya hivi karibuni. Rais Biden alipongeza ushirikiano "muhimu zaidi kuliko hapo awali" mnamo mwezi wa Novemba 2023, baada ya kumpokea mwenzake. Marekani imewekeza hasa katika "Lobito corridor", mradi mkubwa wa miundombinu unaounganisha Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Zambia kupitia bandari ya Lobito nchini Angola.

Kujiondoa kwa Angola hivi majuzi kutoka katika Jumuiya ya Nchi Zinazouza Mafuta kwa Nje (OPEC), huku kukiwa na kutokubaliana kuhusu mgawo wa uzalishaji wa mafuta, pia kumejadiliwa, pamoja na juhudi za Angola kumaliza mzozo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kabla ya Angola, Antony Blinken alizuu Cape Verde, Côte d'Ivoire na Nigeria.

Ziara ya Bw. Blinken inakuja kufuatia ile ya Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi ambaye alizuru Côte d'Ivoire, kituo cha mwisho cha ziara ya Afrika iliyompeleka Misri, Tunisia na Togo. Washington inaichukulia Beijing kuwa mpinzani wake mkuu wa kimkakati na kujionyesha kama mshirika bora wa Afrika kuliko China, ambayo inafadhili miradi mikubwa ya miundombinu kwa mikopo.

Lakini ziara ya mwisho ya rais wa Marekani barani Afrika ni ya mwaka 2015, wakati Barack Obama alipozuru Kenya na Ethiopia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.