Pata taarifa kuu
UCHAGUZI-DEMOKRASIA

Chad kumchagua rais kutamatisha utawala wa kijeshi katika mazingira ya mvutano

Nchini Chad, watu walio katika umri wa kupiga kura wanajiandaa kupiga kura leo Jumatatu Mei 6 katika uchaguzi wa urais unaotarajiwa kuhitimisha kipindi cha mpito kilichodumu kwa miaka mitatu, na baada ya wiki tatu za kampeni za uchaguzi ambazo hatimaye zilizua shauku ya upigaji kura ambayo mawazo yalikuwa "hitimisho lililotangulia", lakini pia mvutano. 

Wananchi wa Chadwanapiga kura kumchagua rais wao, uchaguzi ambao unatamatisha utawala wa kijeshi uliodumu miaka mitatu.
Wananchi wa Chadwanapiga kura kumchagua rais wao, uchaguzi ambao unatamatisha utawala wa kijeshi uliodumu miaka mitatu. © Moussa Alou/ RFI Mandenkan
Matangazo ya kibiashara

Mpito huu utafungwa tu kwa kuanzishwa kwa Bunge la taifa, Bunge la Seneti na mamlaka za mitaa zilizochaguliwa, kulingana na katiba mpya. Tarehe ya chaguzi hizi bado haijatangazwa.

Wagombea kumi wanachuana kuwania nafasi ya juu zaidi katika uchaguzi wa urais nchini Chad, unaofanyika leo Jumatatu Mei 6. Uchaguzi unaotawaliwa na pambano la juu kati ya rais wa kipindi cha mpito, Jenerali Mahamat Idriss Déby, na Waziri Mkuu wake, Succès Masra. Makabiliano haya ambayo hayajawahi kutokea kati ya watu wawili hodari wa Chad yamesababisha sintofahamu.

Uchaguzi huu wa Chad unafuatia kura ya maoni ya katiba iliyofanyika tarehe 17 Desemba 2023, kufuatia kifo cha Rais Idriss Déby mwaka wa 2021. 

Vituo vitafunguliwa mnamo saa moja asubuhi na kufungwa saa kumi na moja jioni. Raia milioni 8.5 wana haki ya kupiga kura kwenye uchaguzi huo wa leo.

Wanajeshi walianza kupiga kura mapema siku ya Jumapili. Matokeo ya awali yanatarajiwa kutangazwa Mei 21 na matokeo kamili yatatolewa Juni 5.

Wanajeshi walianza kupiga kura mapema siku ya Jumapili.
Wanajeshi walianza kupiga kura mapema siku ya Jumapili. © Moussa Alou COULIBALY

Rais wa mpito aliye madarakani Mahamat Déby, mtoto wa hayati rais Idriss Déby, anagombea kwa muhula kamili kama mgombea wa Vuguvugu la ukombozi wa Wazalendo, na hivyo kuwa na uwezekano wa kuongezwa kwa utawala wa miaka 33 wa familia ya Déby.

Rais wa mpito, Mahamat Idriss Déby, atakabiliana, kwa mara ya kwanza, na mtihani wa sanduku la kura wakati wa uchaguzi huu wa urais. Akiwa madarakani tangu Aprili 2021, kiongozi huyo wa sasa alitangazwa kuwa rais na jeshi baada ya kifo cha babake Idriss Deby, aliyeuawa kwenye uwanja wa vita baada ya zaidi ya miaka thelathini ya utawala. Jenerali huyo mwenye umri wa miaka 40 kwa mara ya kwanza aliahidi kurudisha mamlaka kwa raia baada ya kipindi cha mpito cha miezi 18, kabla ya kuongeza muda huu na hatimaye kuingia kwenye kinyang'anyiro hiki.

Wagombea wengine tisa wako kwenye kinyang'anyiro hicho, akiwemo Waziri Mkuu wa zamani Albert Pahimi Padacké, Waziri wa Elimu ya Juu Lydie Beassemda, mwanamke pekee kushindana, lakini pia na zaidi ya yote Waziri Mkuu wa sasa, Succès Masra, ambaye anahudumu kama mpinzani mkuu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.