Pata taarifa kuu
Bahrain

serikali ya Bahrain yatangaza kuunda tume ya wanasheria kupitia hukumu zilizotolewa na mahakama

Serikali ya Bahrain kwa mara ya kwanza imetangaza kuunda tume maalumu ya wanasheria kwa ajili ya kupitia upya baadhi ya hukumu ambazo zimetolewa na mahakama za kijeshi kufuatia maandamano ya mwaka uliopita.

mfalme wa Bahrain Hamad Al-Khalifa
mfalme wa Bahrain Hamad Al-Khalifa Reuters/Stephanie McGehee
Matangazo ya kibiashara

Hatua hiyo imetokana na mapendekezo ya tume maalumu iliyoundwa na serikali mwaka jana kuchunguza mauaji yanayotuhumiwa kutekelezwa na polisi wakati wa maandamano ya kuupinga utawala wa nchi hiyo.

Mpaka sasa mahakama za kijeshi nchini humo zimetoa hukumu tano za watu kunyongwa hatua iliyolazimu tume hiyo kuundwa kuchunguza uhalali wa hukumu hizo na watu wanaoendelea kushikiliwa kwenye magereza mbalimbali nchini humo.

Mwishoni mwa mwaka jana tume maalumu iliyoundwa na mfalme Hamad-Bin-Isa-Al-Khalifa ilikabidhio ripoti yake na kubainisha kuwa polisi walitumia nguvu kubwa katika kukabiliana na waandamanaji huku pia ikieleza kuwa kuna wanaharakati wanashikiliwa kimakosa na polisi.

Serikali ya marekani hivi karibuni ilisema kuwa itaiuzia silaha za kijeshi nchi hiyo kulingana na utekelezaji wa mapendekezo ya tume iliyoundwa na serikali kuchunguza vurugu za nchini humo.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.