Pata taarifa kuu
SYRIA-URUSI-MAPIGANO-USALAMA

Askari wa Urusi kushiriki katika mapigano nchini Syria

Askari wa Urusi wameanza kushiriki katika vita nchini Syria ili kuisaidia serikali ya Rais Bashar Al Assad, vyanzo kadhaa vya Lebanon vimearifu kutokana na hali ya kisiasa na kijeshi inayoendelea kushuhudiwa nchini humo.

Waziri wa mambo ya nje wa Urusi, Sergei Lavrov. Moscow inathibitisha uwepo wa wataalam wa kijeshi nchini Syria lakini inahakikisha kuwa wapo huko tu kusaidia mamlaka kuchukua silaha ilizoletewa. Vyanzo vya Lebanon vinathibitisha kwambasema askari wa Urusi
Waziri wa mambo ya nje wa Urusi, Sergei Lavrov. Moscow inathibitisha uwepo wa wataalam wa kijeshi nchini Syria lakini inahakikisha kuwa wapo huko tu kusaidia mamlaka kuchukua silaha ilizoletewa. Vyanzo vya Lebanon vinathibitisha kwambasema askari wa Urusi REUTERS/Grigory Dukor
Matangazo ya kibiashara

Kwa mujibu wa vyanzo vya Marekani, Urusi imetuma nchini Syria masaa machache yaliyopita meli mbili zilizobeba magari ya kijeshi na ndege za ziada pamoja na kikosi kidgo cha wa nchi kavu na majini.

Afisaa wa waasi wa Syria alisema awali kwamba idadi ya washauri wa kijeshi kutoka Urusi waliongezeka katika kipindi cha mwaka uliyiopita.

Kwa mujibu wa afisaa wa Marekani, Urusi huenda ikaendesha shughuli mbalimbali katika uwanja mdogo wa ndege ilio karibu na bandari ya Latakia, ngome kuu ya vikosi vinavyomuunga mkono Rais Bashar Al Assad, ambavyo vilipata hasara kubwa miezi ya hivi karibuni.

Moscow imehakikisha kuwa kuna wataalam wake wakijeshi waliotumwa katika uwanja wa mapigano, lakini imethibitisha kwamba wataalam wake hao hawashiriki katika vita. Damascus pia imethibitisha kwamba washauri wa kijeshi kutoka Urusi hawashiriki moja kwa moja katika shghuli yoyote ya kijeshi nchini Syria.

Urusi ina kambi ya jeshi la majini katika bandari ya Tartus, Urithi wa Soviet katika zama hizo.

Kwa mujibu wa vyanzo viwili vya Lebanon, ambavyo havikutaka kutajwa, Urusi inajaribu kuweka kambi mbili nchini Syria, moja karibu na pwani, nyingine katika mjoa ya mikoa ya Syria.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.