Raia wa Palestina zaidi ya laki moja wametoroka katika mji wa Rafah
Watu zaidi ya Laki Moja, wamekimbia kutoka kwenye mji wa Rafah, ulipo kwenye ukanda wa Gaza, kuhofia mashambulio ya jeshi la Israeli, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.
Imechapishwa:
Tangazo la kukimbia kwa wakaazi wa Rafah, linakuja wakati huu kundi la Hamas likisema, mazungumzo na Israeli kujaribu kutafuta mkataba, yaliyokuwa yanaendelea jijini Cairo, yamekwama, na wajumbe wake wameondoka.
Aidha, viongozi wa kundi hilo wamesema baada ya mwafaka kutopatikana, hatima ya upatikanaji wa mkataba wa kusitisha vita kwenye ukanda wa Gaza, ipo mikononi mwa Israeli.
Soma piaWaelfu ya watu waendelea kuutoroka mji wa Rafah kufuatia mashambulizi ya jeshi la Israel
Wanajeshi wa Israeli nao wameendelea kurusha mabomu kwenye mji wa Rafah, huku afisa wa Juu wa Umoja wa Mataifa akisema, operesheni za kutoa misaada ya kibinadamu kwa sasa imeshindikana.
Licha ya wito wa Jumuiya ya Kimataifa kuitaka Israel kutoendelea na operesheni yake mjini Rafah na hata Marekani kusema haitotuma silaha kusaidia operesheni hiyo, kwa hofu ya kuwauwa rais wasiokuwa na hatia.
As Israeli Forces bombardment intensifies in #Rafah, forced displacement continues.@UNRWA estimates around 110,000 people have now fled Rafah looking for safety. But nowhere is safe in the #GazaStrip & living conditions are atrocious.
— UNRWA (@UNRWA) May 10, 2024
The only hope is an immediate #Ceasefire pic.twitter.com/gZ4QwetlBF
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema, nchi yake itasimama peke yake, hata kama haitopokea msaada wa nje, na kusisitiza kuwa itaendelea na mpango wake wa kuishambulia Rafah.
Katika hatua nyengine katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani shambulio katika makao makuu wa shirika la UN kuhusu wakimbizi wa Palestina UNRWA.
I condemn the recent attack on @UNRWA's Headquarters in East Jerusalem.
— António Guterres (@antonioguterres) May 10, 2024
Targeting aid workers and humanitarian assets is unacceptable, and must stop. https://t.co/xqVG6e3tOh