UINGEREZA-EU-USHIRIKIANO-SIASA
Theresa May kuomba kuongezwa muda wa nchi yake kujiondoa EU
Waziri Mkuu wa Uingereza Bi Theresa May anatarajiwa kuwaandikia barua wakuu wa Umoja wa Ulaya, kuwoamba, waiongoezee muda nchi yake, kuelekea kujiondoa kwenye Umoja huo.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Hatua hii inakuja, baada ya wabunge kukataa mapendekezo ya serikali yake ya namna ya kujiondoa kwenye umoja huo.
Kumeripotiwa mvutano katika baraza la mawaziri, huku kukiwa na wasiwasi kuwa huenda Uingereza ikachelewa kujiondoa hata kwa muda wa miaka miwili.
Michel Barnier amekuwa akiwakilishaa Umoja wa Ulaya kwenye mazungumzo ya Uingereza kujiondoa.