Pata taarifa kuu

Meli mbili za mizigo zagongana kusini mwa Sweden, watu kadhaa watoweka

Meli mbili za mizigo ziligongana mapema usiku, Jumatatu asubuhi, Desemba 13, kusini mwa Sweden, na kusababisha kupinduka kwa meli moja na mabaharia wawili kuzama baharini, kulingana na mamlaka ya baharini ya Sweden.

Tukio hilo lilitokea katika eneo la Bahari ya Baltic kati ya mji wa pwani ya kusini mwa Sweden wa Ystad na kisiwa cha Denmark Bornholm, Mamlaka ya Bahari ya Uswidi (SMA) ilisema
Tukio hilo lilitokea katika eneo la Bahari ya Baltic kati ya mji wa pwani ya kusini mwa Sweden wa Ystad na kisiwa cha Denmark Bornholm, Mamlaka ya Bahari ya Uswidi (SMA) ilisema REUTERS/Mikko Stig/Lehtikuva
Matangazo ya kibiashara

Ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa 2:30 saa za kimataifa, katika Bahari ya Baltic kati ya ncha ya kusini ya Sweden na kisiwa cha Denmark cha Bornholm kati ya meli ya mizigo ya Uingereza na meli ya Denmark, ambayo ndiyo iliyopinduka,  msemaji wa mamlaka hiyo, Carl- Johan Linde ameliambia shirika la habari la AFP.

Watu kadhaa wanahofiwa kuwa majini na operesheni kubwa ya uokoaji inaendelea, shirika la utangazaji la umma la Uswidi SVT liliripoti Jumatatu

Operesheni kubwa ya uokoaji inayohusisha boti tisa na helikopta inaendelea, katika maji baridi sana, yenye digrii nne tu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.