Pata taarifa kuu
UHISPANIA-UCHAGUZI-SIASA

Vyama vipya vyatazamiwa kushiriki katika mfumo wa utawala Uhispania

Raia wa Uhispania waliitwa Jumapili Mei 24 kuwachagua wawakilishi wao wa manispaa na mikoa. Uchaguzi huu ni muhimu kwa nchi hiyo, ambayo imeanza kuweka sawa mazingira yake ya kisiasa, kwa kuvishirikisha vyama vipya, ikiwa ni pamoja na Podemos na Cuidadanos, hali ambayo inalenga kukomesha mfumo wa utawala wa vyama viwili uliyokua ukijiri nchini humo.

Wafuasi wa chama kipya cha Podemos washeherekea mafanikio ya chama chao katika uchaguzi wakati wa kampeni za uchaguzi, Madrid, Mei 24.
Wafuasi wa chama kipya cha Podemos washeherekea mafanikio ya chama chao katika uchaguzi wakati wa kampeni za uchaguzi, Madrid, Mei 24. REUTERS/Andrea Comas
Matangazo ya kibiashara

Chama cha mrengo wa kulia kiliyo madarakani kinaongoza katika uchaguzi huo, lakini kimepata kura zisiyoridhisha tangu kiingiye madarakani mwaka 1991.

Mazingira ya kisiasa nchini Uhispania yamekua na motisha kufuatia uchaguzi huu wa manispaa na mikoa. chama tawala cha PP kimeanguka kwa kiasi kikubwa katika maeneo mengi na katika taasisi za wawakilishi katika mikoa.

Mshangao mkubwa, kwa sasa, ni kwamba chama cha Podemos kinaweza kuongoza Halmashauri ya jiji la Madrid, baada ya kuchukua nafasi ya pili kikiwa karibu na chama kiliyo madarakani cha mrengo wa kulia.

Mahali pengine, kama katika miji ya Coruna, Saragosse, Seville na Cadix, kumeonekana kuibuka kwa vyama viwili vipya, Podemos na Ciudadanos. Chama cha Podemos kimepata asilimia 20 za kura huku chama cha Ciudadanos kikipata asilimia 10 za kura.

Vyama vingine vipya vimepata kura za kutosha, na hivyo kuweka kikomo kwa mfumo wa utawala wa vyama viwili uliyopangwa katika siasa za Uhispania tangu kuanza kwa mfumo wa demokrasia miaka 40 iliyopita.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.