Pata taarifa kuu
SUDAN-Siasa

Sudan: Mariam al-Mahdi aachiliwa huru

Shirika la habari la SUNA nchini Sudan - limesema mwanasiasa mmoja mashuhuri wa upinzani ameachiwa huru baada ya kushikiliwa kwa mwezi mmoja.

Mariam Sadek al-Mahdi, du parti Umma, lors d'une conférence de presse à Omdurman, le 31 mars 2010.
Mariam Sadek al-Mahdi, du parti Umma, lors d'une conférence de presse à Omdurman, le 31 mars 2010. AFP / E. Hamid
Matangazo ya kibiashara

Shirika hilo la habari limesema naibu mwenyekiti wa chama cha upinzani cha Umma, Mariam Sadek al-Mahdi, ameachiwa huru jumanne wiki hii.

Alikuwa korokoroni kwa muda wa siku 28 katika jela ya wanawake la Omdurman, baada ya vikosi vya usalama kumkamata katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Khartoum Agosti 11 iliyopita.

Alikuwa akirejea nyumbani kutoka Paris ambako alikuwa na mazungumzo ya kusaka umoja pamoja na wapinzani wa rais Omar al-Bashir.

Kiongozi wa chama cha upinzani cha Umma,Sadek al-Mahdi (kushoto)  akiwa pamoja na Yasir Arman (kulia) wa SPLM, wa vyama vya upinzani
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Umma,Sadek al-Mahdi (kushoto) akiwa pamoja na Yasir Arman (kulia) wa SPLM, wa vyama vya upinzani Photo : Zohra Bensemra/ Reuters

Baba yake Sadek al-Mehdi, mwenyekiti wa chama cha upinzani cha Umma, Sadek al Mehdi pia alikamatwa  mapema mwaka huu baada ya kuvilaumu vikosi vya serikali kuhusika na visa vya ukiukaji wa haki za binaadamu katika jimbo la Darfur, kufuatia  kuzuka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe  mwaka 2003.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.