Kijiji cha Bamba chadhibitiwa na makundi yenye silaha
Tangu siku za hivi karibuni, makundi yenye silaha yamekua yakionekana kwa mara nyingine tena katika maeneo ya kaskazini mwa Mali.
Imechapishwa:
Kulikuwa na uporaji, huku milio ya risasi ikisikika katika eneo hilo la kaskazini mwa Mali. lakini wakati huu usalama wa kijiji cha Bamba, kaskazini ya mji wa Gao, unalindwa na makundi mawili ya wanamgambo wa kikabila , ambayo yameyadhibiti maeneo ya mji huo.
Kikiwa kwenye umbali wa kilomita 245 kaskazini mwa mji wa Gao, katika eneo ambapo idadi ya askari ilikua ndogo, kijiji cha Bamba kiko chini ya himaya ya makundi mawili yenye silaha yenye uhusiano wa karibu na serikali ya Mali.
Makundi hayo yaliyotwaa udhibiti wa kijiji cha Bamba ni Gatia pamoja na MAA. Kundi la Gatia lina wanamgambo wengi kutoka jamii ya Watouareg wa Imghad.
Hayo yanajiri wakati ambapo mazungumzo kati ya serikali ya Mali na makundi yenye silaha yanaanza katika mji mkuu wa Algeria, Algiers.